Uncategorised
- Details

Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki Dkt. Msafiri Joseph Mbilu amewakumbusha Wakristo kukemea matendo maovu ambayo yanajitokeza katika jamii hususani mmomonyoko wa maadili katika jamii ikiwemo suala la mapenzi ya jinsia moja.
- Details
Ufunuo 14:13 “Nikasikia sauti kutoka mbinguni ikisema, Andika, Heri wafu wafao katika Bwana tangu sasa. Naam, asema Roho, wapate kupumzika baada ya taabu zao; kwa kuwa matendo yao yafuatana nao”.

Picha za matukio mbalimbali ya Ibada ya Mazishi ya Mwalimu Wahaki Tawi Vesso, iliyofanyika leo tarehe 27/05/2023 katika Jimbo la Pwani Usharika wa Kana, Ibada hii iliongozwa na Baba Askofu Dkt. Msafiri Joseph Mbilu, mwili wa Mwalimu Wahaki Tawi Vesso umezikwa katika makaburi yaliyopo Gofu-Goseji-Tanga,
- Details

TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI..
UTANGULIZI
Tarehe 19 Juni 1963, Kanisa la Usambara - Digo na makanisa mengine sita ya Kilutheri yaliungana na kuunda Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT). Leo hii KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki (KKKT-DKMs) ni miongoni mwa Dayosisi 27 ndani ya KKKT. Dayosisi inaitwa hivyo kwakuwa inapatikana Kaskazini Mashariki mwa Tanzania katika Mkoa wa Tanga. Kwahiyo KKKT-DKMs ni taasisi ya kidini iliyosajiliwa tarehe 19 Juni 1963 na Makao yake Makuu yapo Wilaya ya Lushoto Mkoa wa Tanga. Dhamira ya KKKT-DKMs ni kufundisha na kuhubiri neno la Mungu na kutoa huduma nzuri kiroho, kimwili, kiakili, kiuchumi na kijamii kwa watu. Taasisi hii inatoa tangazo la kazi kwa nafasi ifuatayo:
Sifa za waombaji ni kama ifuatavyo;
- DAKTARI DARAJA LA II (NAFASI 2)
Waombaji wawe na Shahada ya Udaktari wa binadamu kutoka Vyuo vikuu/ Vyuo vinavyotambuliwa na Serikali. Waombaji wawe wamemaliza mafunzo ya kazi “internship” ya muda usiopungua mwaka mmoja na kupata usajili kutoka Baraza la Madaktari Tanganyika (Medical Council of Tanganyika)
- Details
Uongozi wa Taasisi ya Kolowa Technical Training Institute (KOTETI) iliyopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Lushoto-Tanga, yenye usajili namba KOTETI/HAS/249 unapenda kuwatangazia nafasi za masomo kwa muhula mpya 2023/2024 kwa kozi ya famasia yaani Diploma in Pharmaceutical science kwa miaka mitatu (3).
SIFA ZA KUJIUNGA. muombaji awe na kiwango cha alama kuanzia "D" nne (4) na kuendelea katika masomo ya Chemistry na Biology na masomo mengine yoyote mawili isipokuwa ya dini. Ada ni shilingi 1,400,000/= na italipwa kwa awamu. Hosteli nzuri na huduma ya chakula vinapatikana kwa bei nafuu kabisa. Ili kupata fomu za kujiunga ingia kwenye tovuti ya chuo www.koteti.ac.tz au tembelea ofisi za chuo kwa maelezo Zaidi au tuma barua pepe kwa This email address is being protected from spambots. You need JavaScript enabled to view it. au piga simu namba
0712 811 420 au 0747 067 565 au 0784 370 200
Wote mnakaribishwa
Page 52 of 124

