Matukioa katika picha Ibada ya Jumapili ya tarehe 17/09/2023, katika  Usharika wa Źory  nchini Poland, ikiwa ni mwendelezo wa ziara ya Baba Askofu Dkt. Msafiri Joseph Mbilu, ambapo  kutoka Bara la Afrika ni  Mjumbe pekee  kwenye Kamati ya Ibada na Muziki kwenye mkutano Mkuu wa Fungamano la Makanisa ya Kilutheri Duniani (LWF) unaoendelea nchini Poland .Wajumbe wa Mkutano huo  wamepata nafasi ya kushiriki Ibada ya Jumapili  kwenye sharika mbalimbali. Ujumbe mkuu wa Mkutano huu ni kutoka kitabu cha Waefeso 4:4-6 "MWILI MMOJA, ROHO MMOJA, TUMAINI MOJA".

 
Ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa 13 wa Fungamano la Makanisa ya Kilutheri (LWF) Duniani, ambao ni chombo cha juu cha maamuzi unao ongozwa na kauli mbiu isemayo MWILI MMOJA, ROHO MMOJA, TUMAINI MOJA “Waefeso 4:4-6”. unafunguliwa katika Mji wa Krakow Poland leo tarehe 13/09/2023.
Mkutano huu utakuwa na jukumu la kumchagua Rais mpya wa Fungamano na Wajumbe wa Kamati mbalimbali. Rais anayemaliza muda wake ni Askofu Dkt. Panti Filibus Musa wa Kanisa la Kilutheri Nigeria.
 
Kutoka Bara la Afrika, Askofu Dkt. Msafiri Joseph Mbilu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki ni Mjumbe wa Kamati ya Ibada na Muziki iliyoteuliwa kuandaa Mkutano huu na atashiriki kuongoza nyimbo za utamaduni wa Kiafrika.Kamati hii iliundwa mwaka 2021 na ofisi ya Katibu Mkuu wa Fungamano la Makanisa ya Kilutheri Duniani ambayo makao Makuu yake yapo Geneva Uswis. Kamati hii ina wajumbe kumi kutoka Ujerumani,Canada,Norway,Hungary,Poland,Hong Kong,USA,Brazil,Switzeland na Africa ambapo mjumbe muwakilishi ni Askofu Dkt. Msafiri Mbilu. 
 
Hata hivyo, Mkuu wa KKKT Baba Askofu Dkt. Fredrick Onael Shoo anawakilisha Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania akiambatana na Katibu Mkuu KKKT Mhandisi Robert Kitundu na wajumbe wengine 10 kutoka makundi mbalimbali kama vile Vijana na Wanawake.
 
 

Leo tarehe 02 Septemba,2023, Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, Mch Dkt. Msafiri Joseph Mbilu,amemtembelea Dean Mstaafu  wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki Mch. Amasia Mweta, nyumbani kwake Mpalalu-Bumbuli.

Tarehe 27/08/2023 imekuwa siku ya baraka tele kwa washarika wa Jimbo la Kusini ,Usharika wa Irente kwani vijana wapatao 36 wamebarikiwa huku mmoja kati yao akibatizwa. Baba Askofu Dkt. Msafiri Joseph Mbilu ndiye aliyeongoza Ibada hiyo. Katika Risala ya vijana hao waliobarikiwa kwa Baba Askofu Dkt. Mbilu , wamekiri kufundishwa Biblia kwa ujumla wake , mtaala wa kitabu cha pokea chapa ya Kristo na vitabu vingine, katekisimo ndogo ya Martin Luther , nyimbo za Ibada na Liturgia katika kitabu cha Tumwabudu Mungu Wetu na kuahidi kuwa imani yao sasa ni thabiti na kamwe hawata tikiswa na ulimwengu na wataendelea kuwa wafuasi na wanafunzi chini ya mwalimu mkuu yaani Yesu Kristo hadi hapo atakaporudi kulichukuwa kanisa lake.