Askofu  wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, Mch.Dkt Msafiri Joseph Mbilu leo Tarehe 25/12/2021 ameongoza Ibada katika Kanisa Kuu (Cathedral) Lushoto.Ikiwa leo ni sikukuu ya Krismas Baba Askofu Mbilu amehubiri neno la Mungu kutoka kitabu cha Luka 2:10 nalo linasema “Malaika akawaambia, Msiogope; kwa kuwa mimi ninawaletea habari njema ya furaha kuu itakayokuwa kwa watu wote”.

Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, Mch Dkt. Msafiri Joseph Mbilu ameongoza Ibada ya mazishi ya marehemu Mzee Enock Nickodem Magombya Leo tarehe 22/12/2021 katika Usharika wa Hale Jimbo la Tambarare.

Nyumba hubarikiwa ukaamo,Yesu,uliye mpenzi wa moyo,wakukaribishapo kwa furaha,uliye mgeni wa heshima kuu.mioyo yetu inapokupenda na macho Yote yakungojapo, midomo yote ikuulizapo, na watu wote wanapokutii.