Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, Mch Dkt. Msafiri Joseph Mbilu amewapongeza nakuwatakia baraka za Mungu katika masomo yao wanafunzi wanaoenda masomoni kwa mhula mpya wa masomo na wale ambao wanaendelea na masomo katika Chuo cha Biblia na Theolojia Mwika pamoja na Chuo Kikuu cha Tumaini Makumira.

Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki Mch Dkt. Msafiri Joseph Mbilu ameongoza Ibada iliyokuwa na tendo la kuzindua Jimbo la tano ndani ya KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki,Ibada hiyo pia iliambatana na kuingizwa kazini kwa Mkuu wa Jimbo hilo Mch. Ishmael Reuben Ngoda pamoja na Katibu Mkuu wa Dayosisi Mwl. Julius Samwel Madiga .

Msaidizi wa Askofu KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki Mch. Michael Mlondakweli Kanju amewataka Washarika wa Usharika wa Mkata na wakristo kwa ujumla kumuamini Mungu na kumpa nafasi katika maisha yao pindi wanapokutana na changamoto mbalimbali katika maisha, na kuacha tabia iliyozuka katika jamii ya kujitoa uhai.