ELCT North Eastern Diocese
Msaidizi wa Askofu Atoa Wito kwa Halmashauri Mpya ya Mipango na Fedha KKKT-DKMs
- Details

Habari kwa Ufupi Lushoto, Tanga – Msaidizi wa Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania, Dayosisi ya Kaskazini Mashariki (KKKT-DKMs), Mch. Frank Richard Mntangi, amewataka wajumbe wa Halmashauri mpya ya Mipango na Fedha ya KKKT-DKMs kuweka mbele maslahi mapana ya Dayosisi katika utekelezaji wa majukumu yao. Amesisitiza kuwa Halmashauri hii ni "moja ya moyo wa maendeleo" ndani ya Dayosisi.
- Hits: 3536
Askofu Dkt. Mbilu akutana na kufanya mazungumzo na Viongozi wa juu wa UEM
- Details

#HABARI: Juni 23, 2025, Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, Dkt. Msafiri Joseph Mbilu ameendelea na ziara yake ya kikazi nchini Ujerumani na amekuwa na vikao muhimu sana vinavyolenga kuimarisha ushirikiano kati ya KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki na UEM, pamoja na kujadili fursa za maendeleo na ushirikiano katika nyanja mbalimbali.
Kwa nyakati tofauti Baba Askofu Dkt. Msafiri Mbilu, amekuwa na vikao na Katibu Mkuu wa UEM, Mch. Dkt. Andar Parlindungan, Naibu Katibu Mkuu UEM anayesimamia Bara la Africa Mch. Dkt. John Wesley Kabango, Mkurugenzi wa Fedha wa UEM, Bwana Timo Pauler pamoja na iliyewahi kuwa meneja wa shamba la Irente farm miaka ya 1991 na kuendelea Bwana Mr. Jeans Pfeil .
UEM: United Evangelical Mission ni chama Cha kiinjili Cha kimisioni kilicho anzishwa mnamo mwaka 1996 na Wamisionari kutoka Ujerumani wa Rhenish na Betheli ambao walifika Africa, na Asia kwa ajili ya kuanzisha shughuli za Dini. Katika Africa walifika katika nchi 7 ambazo ni Tanzania, DR Congo, Africa ya Kusini, Botswana, Cameroon, Namibia na Rwanda kukiwa na madhehebu 15. Katika Tanzania UEM inawakilishwa na Makanisa 4 ya KKKT ambayo ni KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Magharibi, KKKT-Dayosisi ya Mashariki na Pwani pamoja na KKKT-Dayosisi ya Karagwe.
- Hits: 4772
Page 4 of 132



