ELCT North Eastern Diocese
Mch. Frank Richard Mntangi Dean Mteule KKKT-DKMs
- Details
Wajumbe 217 kati ya 246 wa Mkutano Mkuu wa tano (5) baada ya Jubilee ya miaka 125 ya Injili KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki (KKKT-DKMs) sawa asilimia 88.5% wamemuidhinisha Mchungaji Frank Richard Mntangi kuwa Msaidizi wa Askofu (Dean Mteule) wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki.
Mch. Frank Mntangi ambaye kwa sasa ni Mkuu wa Jimbo la Pwani, ameteuliwa kuhudumu nafasi hiyo ya msaidizi wa Askofu ambayo kwa sasa inaongozwa na Mch. Michael Mlondakweli Kanju anayestaafu kwa mujibu wa sheria za utumishi za KKKT- Dayosisi ya Kaskazini Mashariki.
- Hits: 2823
Askofu Dkt. Mbilu ziarani Shule ya Sekondari Lwandai
- Details

- Hits: 3305
Pumzika kwa Amani Mama Askofu Elfriede Sebastian Kolowa
- Details
KATIKA PICHA:Mazishi ya Mama Askofu Elfriede Sebastian Kolowa iliyofanyika KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki,Usharika wa Kanisa Kuu Lushoto leo tarehe 06/03/2025. Ibada hii iliongozwa na Mkuu wa KKKT Baba Askofu Dkt. Alex Gehaz Malasusa.Marehemu, Bibi Elfriede Sebastian Kolowa alizaliwa tarehe 30 mwezi Juni mwaka 1934 huko Bumbuli Salem Wilaya ya Lushoto Mkoa wa Tanga akiwa Mtoto wa 6 wa Mwalimu Emmanuel Chamshama na Bibi Sarah Shemshi.Mwili mwili wake umepumzishwa leo tarehe 06/03/2025 katika makaburi yaliyopo katika eneo la Kanisa Kuu Lushoto.Sehemu ya historia ya Bibi Elfriede Sebastian Kolowa inaeleza kuwa.
- Hits: 3327
Tangazo la kazi Mratibu wa Kituo cha Maendeleo ya Mtoto
- Details
Tarehe 19 Juni 1963, Kanisa la Usambara - Digo na makanisa mengine sita ya Kilutheri yaliungana na kuunda Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania . Leo hii KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki (KKKT-DKMs) yenye Makao Makuu Wilayani Lushoto Mkoani Tanga ni miongoni mwa Dayosisi 28 za KKKT. Dayosisi inaitwa hivyo kwakuwa inapatikana Kaskazini Mashariki mwa Tanzania katika Mkoa wa Tanga. Kwahiyo KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki (KKKT-DKMs) ni taasisi ya kidini iliyosajiliwa tarehe 19 Juni 1963 na Makao yake Makuu yapo Wilaya ya Lushoto Mkoa wa Tanga. Dhamira ya KKKT-DKMs ni kufundisha na kuhubiri neno la Mungu na kutoa huduma nzuri za kiroho, kimwili, kiakili, kiuchumi na kijamii kwa watu wote. Taasisi hii inatoa tangazo la kazi kwa nafasi moja ya MRATIBU WA HUDUMA YA MTOTO NA KIJANA (PROJECT COORDINATOR) kwa vijana wote (Wakristo)
NAFASI NA WAJIBU WA MRATIBU WA HUDUMA YA MTOTO NA KIJANA (PROJECT COORDINATOR).
1.1 CHILD AND YOUTH DEVELOPMENT CENTER COORDINATOR (CYDC)- MRATIBU WA KITUO CHA MAENDELEO YA MTOTO NA KIJANA.
- Hits: 3263
Page 4 of 129