ELCT North Eastern Diocese
Askofu Dkt. Mbilu apokea ugeni kutoka Vyuo vitano ,vya Muhimbili(MUHAS),KCMC/KCMU,Chuo cha Kenyata
- Details
Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki Dkt. Msafiri Joseph Mbilu amepokea ugeni maalum kutoka Vyuo vikuu vitano ambavyo ni, Muhimbili (MUHAS), KCMC/KCMU,Chuo cha Kenyata kilichopo Kenya,Chuo cha Protoria cha Africa ya Kusini na Chuo kikuu cha Leibniz kilichopo Hannover Ujerumani, uliokuja kwa lengo la kutembelea vituo mbalimbali vinavyomilikiwa na KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki ili kuanzisha umoja wa Vyuo hivyo na Taasisi ya Kolowa Technical Training Institute (KOTETI) kwa madhumuni ya kuanzisha kozi ya lugha na mawasiliano ( Speech and language therapy).
- Hits: 1891
Askofu Dkt. Mbilu awataka wakristo kukemea matendo maovu yanayojitokeza katika jamii
- Details
Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki Dkt. Msafiri Joseph Mbilu amewakumbusha Wakristo kukemea matendo maovu ambayo yanajitokeza katika jamii hususani mmomonyoko wa maadili katika jamii ikiwemo suala la mapenzi ya jinsia moja.
- Hits: 1966
Pumzika kwa Amani Mwalimu Wahaki Tawi Vesso
- Details
Ufunuo 14:13 “Nikasikia sauti kutoka mbinguni ikisema, Andika, Heri wafu wafao katika Bwana tangu sasa. Naam, asema Roho, wapate kupumzika baada ya taabu zao; kwa kuwa matendo yao yafuatana nao”.
Picha za matukio mbalimbali ya Ibada ya Mazishi ya Mwalimu Wahaki Tawi Vesso, iliyofanyika leo tarehe 27/05/2023 katika Jimbo la Pwani Usharika wa Kana, Ibada hii iliongozwa na Baba Askofu Dkt. Msafiri Joseph Mbilu, mwili wa Mwalimu Wahaki Tawi Vesso umezikwa katika makaburi yaliyopo Gofu-Goseji-Tanga,
- Hits: 2150
Tangazo la nafasi ya kazi Daktari daraja la 2
- Details
TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI..
UTANGULIZI
Tarehe 19 Juni 1963, Kanisa la Usambara - Digo na makanisa mengine sita ya Kilutheri yaliungana na kuunda Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT). Leo hii KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki (KKKT-DKMs) ni miongoni mwa Dayosisi 27 ndani ya KKKT. Dayosisi inaitwa hivyo kwakuwa inapatikana Kaskazini Mashariki mwa Tanzania katika Mkoa wa Tanga. Kwahiyo KKKT-DKMs ni taasisi ya kidini iliyosajiliwa tarehe 19 Juni 1963 na Makao yake Makuu yapo Wilaya ya Lushoto Mkoa wa Tanga. Dhamira ya KKKT-DKMs ni kufundisha na kuhubiri neno la Mungu na kutoa huduma nzuri kiroho, kimwili, kiakili, kiuchumi na kijamii kwa watu. Taasisi hii inatoa tangazo la kazi kwa nafasi ifuatayo:
Sifa za waombaji ni kama ifuatavyo;
- DAKTARI DARAJA LA II (NAFASI 2)
Waombaji wawe na Shahada ya Udaktari wa binadamu kutoka Vyuo vikuu/ Vyuo vinavyotambuliwa na Serikali. Waombaji wawe wamemaliza mafunzo ya kazi “internship” ya muda usiopungua mwaka mmoja na kupata usajili kutoka Baraza la Madaktari Tanganyika (Medical Council of Tanganyika)
- Hits: 2277
Page 7 of 91