ELCT North Eastern Diocese
Toggle Navigation
  • Home
  • Our Diocese
  • Wopa
  • Gallery
  • Institutions
    • Irente Children's Home
    • Irente School for the Blind
    • Rainbow School
    • Lwandai Secondary School
    • Lutindi Mental Hospital
    • Bangala Lutheran Junior Seminary
    • Bumbuli Hospital
    • SEKOMU university
    • Namna ya kuchangia kazi za maendeleo na Vituo vya kutoa huduma kwa watu wenye mahitaji maalumu (KKKT-DKMs)
  • Calendar
  • Projects
    • Irente Biodiversity Reserve
    • UTC - Usambara Technological Center
    • Restaurants and Hostels
      • Tumaini Mbuyukenda Hostel and Restaurant
      • Martin Luther Garden and Restaurant
      • Tumaini Songe Restaurant and Hostel
      • Hohen Restaurant and Hostel
      • Tumaini Lushoto Restaurant and Hostel
  • Superintendent
    • Coast Superintendent
    • Northern Superintendent
    • Southern Superintendent
    • Plains Superintendent
  • New-clips
  • Contact us
  • You are here:  
  • Home

Bishop Rev.Dr. Msafiri J. Mbilu

Change Language

English German Spanish Swahili Swedish

News & Updates

  • TANGAZO LA NAFASI MOJA YA KAZI MENEJA WA SHAMBA (FARM MANAGER) KITUO CHA IRENTE FARM

    TANGAZO LA NAFASI MOJA YA KAZI MENEJA WA SHAMBA (FARM MANAGER) KITUO CHA IRENTE FARM

    TANGAZO LA NAFASI YA KAZI Tarehe 19 Juni 1963, Kanisa la Usambara - Digo na makanisa mengine sita ya...
  • Askofu Dkt.Mbilu akutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi wa Uendeshaji  NSSF

    Askofu Dkt.Mbilu akutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi wa Uendeshaji NSSF

    Leo tarehe 01/04/2026, Askofu Dkt. Msafiri Joseph Mbilu amepokea ugeni kutoka Mfuko wa Taifa wa Hifa...
  • TAARIFA

    TAARIFA

    Uongozi wa KKKT – Dayosisi ya Kaskazini Mashariki ukiwakilishwa na Katibu Mkuu Mwl. Julius Madiga, u...
  • ASKOFU KKKT DAYOSISI YA KASKAZINI MASHARIKI AZINDUA BODI YA MFUKO WA PENSION

    ASKOFU KKKT DAYOSISI YA KASKAZINI MASHARIKI AZINDUA BODI YA MFUKO WA PENSION

    Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki. Dkt. Msafiri Jos...
  • Taarifa Ziara ya Botswana kwenye Mkutano wa UEM Kanda ya Afrika

    Taarifa Ziara ya Botswana kwenye Mkutano wa UEM Kanda ya Afrika

    Dayosisi yetu imepata heshima kubwa ya kushiriki katika Mkutano wa Kanda ya Afrika ulioandaliwa na U...

.



 

 

Staff Email

ELCT North Eastern Diocese

Askofu Dkt. Mbilu aweka wakfu pikipiki rasmi kutumika Idara ya Mashamba

  • Print
Details
Published: 28 January 2026

 

Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, Dkt. Msafiri Joseph Mbilu, ameongoza Ibada ya kuweka  wakfu chombo cha usafiri (pikipiki) na kumkabidhi kadi ya pikipiki pamoja na ufunguo Mkurugenzi wa Kurugenzi ya Uchumi, Mipango na Maendeleo, Bi. Pendo Lauwo, kwa ajili ya shughuli za kikazi za kila siku za Idara ya Mashamba.

Ibada hiyo pamoja na makabidhiano hayo yamefanyika tarehe 28/01/2025 katika Ofisi za Makao Makuu ya Dayosisi, Lushoto-Tanga. Chombo hiki cha usafiri kitasaidia katika mazingira ambayo hakuna barabara zinazofikika kwa kutumia usafiri wa gari.

Hits: 2990

Read more ...

Askofu Dkt. Mbilu Aongoza Kikao Kazi cha Wachungaji

  • Print
Details
Published: 13 January 2026

Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki,Dkt. Msafiri Joseph Mbilu, ameongoza kikao kazi cha Wachungaji kilicholenga kuweka mipango yamwaka 2026 na kufanya tathmini ya hali ya Deni la Dayosisi pamoja na kuweka mikakati mipya ya pamoja ya kulikabili na kulimaliza.

Kikao hicho kimefanyika tarehe 13 Januari, 2026 katika Usharika wa Kanisa Kuu Lushoto, kikihusisha Wachungaji kutoka sharika mbalimbali za Dayosisi. Lengo kuu la kikao kilikuwa ni kuimarisha ushirikiano, kuweka mikakati shirikishi,kupanga na kuendeleza mipango ya utekelezaji kwa mwaka 2026, ikiwemo mpango mahsusi wa kumaliza deni la Dayosisi.

Akifungua kikao hicho, Askofu Dkt. Mbilu aliwashukuru kwa dhati Wachungaji, watumishi na Washarika wote wa Dayosisi kwa moyo wa kujitoa na ushiriki wao mkubwa katika kuitenda kazi ya Bwana, hususani katika kuchangia deni la Dayosisi. Alisisitiza umuhimu wa kuendelea kuwa waaminifu, na watu wenye mshikamano na  maono ya pamoja kwa maendeleo ya Kanisa.

 Katika kikao hicho pia kulifanyika zoezi la utoaji wa tuzo ya pongezi kwa moja ya usharika uliofanya vizuri katika uchangiaji wa deni la Dayosisi. Uongozi wa Dayosisi ulimpongeza kwa kipekee Mch. Anna Msisili wa Usharika wa Ubiri pamoja na washarika wa Usharika huo, ambao wamefanikiwa kukamilisha kiwango chote cha uchangiaji wa deni la Dayosisi na kushika nafasi ya KWANZA kati ya sharika 76 za Dayosisi kwa kutimiza lengo kwa wakati.Zoezi hili lilifanyika katika sehemu ya ufunguzi wa kikao hicho.

Tuzo hiyo ilipokelewa na Mchungaji  Anna Msisili, aliyeambatana na Wazee wa Kanisa wa Usharika huo.Tuzo hiyo ni miongoni mwa tuzo zinazotolewa kwa sharika 10 za mwanzo zitakazokamilisha deni kwa wakati, na inabeba ujumbe wa neno la Mungu kutoka Kutoka 33:14 unaosema: “Uso wangu utakwenda pamoja nawe, nami nitakupa raha.”

Aidha, taarifa ya kina kuhusu hali ya uchangiaji wa deni la Dayosisi kwa kila usharika iliwasilishwa kwa Wachungaji na Mkurugenzi wa Fedha na Utawala wa Dayosisi, CPA Peter John Singano. Ilielezwa kuwa taarifa rasmi kwa Washarika wote itatolewa tarehe 18 Januari, 2026, na itasomwa katika sharika.

Hits: 3233

TUZO YA PONGEZI KWA KUCHANGIA DENI LA DAYOSISI

  • Print
Details
Published: 04 January 2026

Hits: 3498

Heri ya Mwaka Mpya 2026

  • Print
Details
Published: 01 January 2026

Hits: 3957
  1. Askofu Dkt. Mbilu Akabidhi Gari 1 kwa Kituo Cha Lutindi Mental Hospital
  2. ELCT-NED FAMILY BONANZA 2025
  3. Askofu Dkt. Mbilu Atamatisha Kalenda ya Matukio 2025, Awashukuru Wanadayosisi kwa Ushirikiano wa Kipekee
  4. Kikao cha Halmashauri ya Kurugenzi ya Huduma za Jamii KKKT-DKMs

Page 3 of 137

  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • ...
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10

Back to Top

© 2026 ELCT North Eastern Diocese