ELCT North Eastern Diocese
Askofu Dkt. Mbilu ziarani nchini Ujerumani
- Details
Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, Mch Dkt. Msafiri Joseph Mbilu, yupo ziarani nchini Ujerumani, ambapo akiwa nchini humo atashiriki Ibada ya kumuaga Katibu Mkuu wa chama Cha kiinjili Cha kimisioni (UEM) anayemaliza muda wake Mch.Volker Dally na kuingizwa kazini kwa Katibu Mkuu mpya wa UEM Mch. Dkt. Andar Parlindungan,ambaye awali alikuwa Katibu mtendaji wa idaraya mafunzona uwezeshajiwa UEM.Ibada itafanyika tarehe 01/03/2024
- Hits: 1316
Kilele mwaka wa Wanawake Askofu Dkt. Mbilu awapongeza kwa kujitoa
- Details
MATUKIO KATIKA PICHA: Ibada ya Jumapili siku ya Bwana ya 5 kabla ya Pasaka siku ya kuondoa ukatili, iliyofanyika KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki Usharika wa Kanisa Kuu Lushoto. Ibada hii ilikuwa na matendo mkuu mbalimbali ikiwemu tendo la kufunga mwaka wa Wanawake wa KKKT-DKMs uliozinduliwa 06/03/2022 pamoja na Jubilee ya miaka 25 ya utumishi ya Mchungaji Alice Kopwe na Mch Neema Kamendu.Ibada iliongozwa na inaongozwa na Baba Askofu Dkt. Msafiri Joseph Mbilu. 25/02/2024. Unaweza kutazama Ibada hii kwa kubonyeza link hii hapa chini.
- Hits: 1343
Habari njema kutoka BUMBULI
- Details
TANGAZO
MGANGA MFAWIDHI WA HOSPITALI YA KILUTHERI YA BUMBULI ILIYOPO KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA BUMBULI MKOANI TANGA INAYOMILIKIWA NA KKKT-DAYOSISI YA KASKAZINI MASHARIKI ANAWATANGAZIA KUWA KUTAKUWA NA ZOEZI LA MATIBABU YA MACHO LITAKALO FANYIKA KUANZIA TAREHE 04-08/03/2024 KATIKA HOSPITALI, ZOEZI HILI LITAFANYWA NA MADAKTARI BINGWA KUTOKA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA TANGA- BOMBO
GHARAMA ZA MATIBABU NI KAMA IFUATAVYO
UANDIKISHAJI WA KADI 3,000
UPASUAJI WA MTOTO WA JICHO 50,000
MIWANI YA KUSOMEA 15,000
DAWA YA MACHO 3,000
- Hits: 1626
Dean Kanju awashukuru wana KKKT-DKMs, awataka kuwapuuza wapotoshaji juu ya Deni la Dayosisi
- Details
Msaidizi wa Askofu, KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki Dean Michael Mlondakweli Kanju amewashukuru Washarika wa Usharika wa Soni Mtaa wa Kwang’wenda kwa namna wanavyoendelea kujitoa kwa hali na mali katika kumtumikia Mungu sambamba na uchangiaji wa deni linaloikabili Dayosisi.
- Hits: 1896
Page 5 of 107