ELCT North Eastern Diocese
Kamati ya amani Wilaya ya Lushoto Mkoani Tanga kuhamasisha jamii kushiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa
- Details

- Hits: 3309
Askofu Dkt. Mbilu atoa wito kwa Watanzania kujitokeza kwa wingi katika vituo vya kujiandikisha
- Details
Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, Dkt Msafiri Joseph Mbilu,amempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kuwa mstari wa mbele katika kuwahamasisha Watanzania kuendelea kujitokeza katika zoezi la kujiandikisha katika daftari la wapigakura huku akiwataka Watanzia wote kutumia muda uliobaki kuendelea kujitokeza katika Vituo mbalimbali vya kujiandikisha kwa kuwa ni wajibu kushiriki katika kuchagua viongozi watakaoweza kuwasaidia wananchi.
Askofu Dkt Mbilu ametoa witu huo leo tarehe 14/10/2024 mara baada ya kujiandikisha kwenye daftari la Wapigakura kwaajili ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa katika Kituo cha kujiandikisha cha Uwalu Wilayani Lushoto Mkoani Tanga na kuwasihi Watanzania wote kuendelea kujitokeza kwa wingi katika kujiandikisha ili kutimiza haki yao ya kimsingi ya kikatiba ya yakupiga kura wakati utakapofika.
- Hits: 3429
Ibada ya Kipaimara Usharika wa Bumbuli , Youths Confirmation at Bumbuli Lutheran Parish
- Details
Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, Dkt Msafiri Joseph Mbilu, ameongoza Ibada ya kuwabariki Vijana wa Kipaimara,uwekwaji wa jiwe la msingi la nyumba ya mtumishi pamoja na Ubatizo, Ibada iliyofanyika katika Jimbo la Kusini Usharika wa Bumbuli leo tarehe 13/10/2024.
- Hits: 3195
Ibada ya Kipaimara Usharika wa Mombo , Youths Confirmation at Mombo Lutheran Parish
- Details
Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, Dkt Msafiri Joseph Mbilu, amewapongeza Washarika wa Usharika Mombo kwa namna wanavyoendelea kujitoa katika kumtumikia Mungu katika kuchangia ulipaji wa deni la Dayosisi pamoja na ujenzi wa Kanisa jipya na la kisasa linaloendelea kujengwa katika Usharika huo.
Ameyasema hayo wakati akitoa salamu zake katika Ibada ya Kipaimara iliyofanyika tarehe 12/10/2024 katika Jimbo la Tambarale Usharika wa Mombo na kuongeza kuwa amefarijika kuona Washarika wa Usharika wa Mombo wanavyojitoa katika kuchangia ulipaji wa deni la Dayosisi na anaamini kwa namna ambavyo kila mmoja anajitoa siku moja deni hilo litakwisha huku akiwasihi kila mmoja kuendelee kujitoa kwa moyo.
- Hits: 3479
Page 8 of 127