ELCT North Eastern Diocese
KOTETI YAANZA UDAHILI KWA MWAKA WA MASOMO 2023-2024 KOZI YA FAMASIA (Pharmacy).
- Details
Uongozi wa Taasisi ya Kolowa Technical Training Institute (KOTETI) iliyopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Lushoto-Tanga, yenye usajili namba KOTETI/HAS/249 unapenda kuwatangazia nafasi za masomo kwa muhula mpya 2023/2024 kwa kozi ya famasia yaani Diploma in Pharmaceutical science kwa miaka mitatu (3).
SIFA ZA KUJIUNGA. muombaji awe na kiwango cha alama kuanzia "D" nne (4) na kuendelea katika masomo ya Chemistry na Biology na masomo mengine yoyote mawili isipokuwa ya dini. Ada ni shilingi 1,400,000/= na italipwa kwa awamu. Hosteli nzuri na huduma ya chakula vinapatikana kwa bei nafuu kabisa. Ili kupata fomu za kujiunga ingia kwenye tovuti ya chuo www.koteti.ac.tz au tembelea ofisi za chuo kwa maelezo Zaidi au tuma barua pepe kwa This email address is being protected from spambots. You need JavaScript enabled to view it. au piga simu namba
0712 811 420 au 0747 067 565 au 0784 370 200
Wote mnakaribishwa
- Hits: 2232
Askofu Dkt. Mbilu azindua Ushirika wa Wanafunzi wa Kikristo wa Vyuo vikuu na vya kati (USCF).
- Details
HABARI PICHA: Picha za matukio mbalimbali ya uzinduzi wa Ushirika wa Wanafunzi wa Kikristo wa Vyuo vikuu na vya kati (USCF) uliofanyika leo tarehe 14/05/2023 katika ukumbi wa Chuo cha Afya na Sayansi Shirikishi Tanga.Baba Askofu Dkt. Msafiri Joseph Mbilu ambaye pia ni Katibu wa CCT Mkoa wa Tanga alimumuingiza kazini Mch. Rogers Chamani wa Kanisa Anglican kuwa Mratibu wa USCF Mkoa wa Tanga.
- Hits: 2389
ASKOFU DKT. MBILU: Tujifunze kuomba kwa usahihi.
- Details
Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, Dkt. Msafiri Joseph Mbilu amewakumbusha Washarika wa Usharika wa Kana na Wakristo kwa ujumla, kuendelea kuomba neema ya Mungu iwaongoze katika kuomba kwa usahihi kama Kristo Yesu alivyo wafundisha wanafunzi wake katika Sala ya Bwana.
Askofu Dkt. Mbilu ametoa wito huo leo tarehe 14/05/2023 wakati akihubiri katika Ibada ya Jumapili ya tano baada ya Pasaka (Rogate) iliyofanyika katika Jimbo la Pwani Usharika wa Kana, ambapo amesema kwa sasa kumekuwa na uwepo wa walimu wanaofundisha mafundisho potofu yanayo wafanya Wakristo kushindwa kuomba kwa usahihi.
- Hits: 2870
Mkutano wa Fungamano la Makanisa ya Kilutheri Duniani,kanda ya Afrika
- Details
KATIKA PICHA ni Ujumbe kutoka Tanzania uliohudhuria Mkutano wa Fungamano la Makanisa ya Kilutheri Duniani. Katikati ni Mkuu wa KKKT Askofu Dkt. Fredrick Shoo, kushoto kwake ni Katibu Mkuu wa LWF Mch. Dkt.. Anne Burghadt akifuatiwa na Rais wa LWF Archibishop Musa Panti Filibus.
- Hits: 2558
Page 8 of 91