ELCT North Eastern Diocese
ELCT-NED FAMILY BONANZA 2025
- Details

ELCT-NED FAMILY BONANZA, lililoratibiwa na Kurugenzi ya Uchumi, Mipango na Maendeleo Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania – Dayosisi ya Kaskazini Mashariki (KKKT-DKMs), limefanyika tarehe 13 Desemba 2025 katika Hoteli ya Mbuyukenda, jijini Tanga, likiwakutanisha waumini, wadau mbalimbali pamoja na familia zao kutoka maeneo mbalimbali.
- Hits: 2175
Askofu Dkt. Mbilu Atamatisha Kalenda ya Matukio 2025, Awashukuru Wanadayosisi kwa Ushirikiano wa Kipekee
- Details

Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki (KKKT-DKMs), Dkt. Msafiri Joseph Mbilu, amewashukuru kwa dhati wanadayosisi wote kwa namna wanavyoendelea kujitoa katika ulipaji wa Deni la Dayosisi, akisisitiza kuwa hatua hiyo imekuwa ikitoa matumaini makubwa katika kufanikisha mpango wa kulimaliza deni hilo.
- Hits: 1947
Kikao cha Halmashauri ya Kurugenzi ya Huduma za Jamii KKKT-DKMs
- Details
![]()
Kikao cha Halmashauri ya Kurugenzi ya Huduma za Jamii – KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki kimefanyika tarehe 05 Desemba 2025 katika ukumbi mdogo wa mikutano wa Utondolo, Lushoto.
Kikao hiki kimeonesha kwa namna ya pekee jinsi Kurugenzi hii inavyotekeleza majukumu yake kwa ufanisi na kusimamia kwa weledi vituo mbalimbali vya huduma ambavyo vimeendelea kuleta manufaa makubwa kwa Kanisa na kwa jamii ya Watanzania kwa ujumla.
Katika kikao hicho, wajumbe walijadili kwa kina mikakati ya kuboresha na kukuza huduma katika vituo vyote vilivyo chini ya Dayosisi. Mkurugenzi wa Huduma za Jamii, Mwl. Afizai Vuliva, aliwasilisha taarifa ya utekelezaji wa majukumu ya Kurugenzi kwa lengo la kupokea ushauri na maoni ya wajumbe. Taarifa hiyo imeonesha hatua kubwa zilizopigwa, changamoto zilizopo, pamoja na maeneo yanayohitaji kuimarishwa ili kuongeza tija na ubora wa huduma kwa Kanisa na jamii kwa ujumla. Kurugenzi ya Huduma za Jamii inasimamia na kuratibu idara muhimu zinazogusa maisha ya Kanisa na Jamii moja kwa moja, zikiwemo:
- Idara ya Elimu
- Idara ya Afya
- Idara ya Jinsia na Watoto
- Diakonia (Huduma za Uangalizi na Uchangiaji kwa Jamii)
- Idara ya Vijana na UKWATA
Kupitia usimamizi makini wa Kurugenzi hii, vituo hivi vya huduma vya Dayosisi vimeendelea kuimarika na kutoa huduma zenye kiwango bora, hivyo kuifanya KKKT – Dayosisi ya Kaskazini Mashariki kuwa mfano wa kuigwa katika utoaji na usimamizi wa huduma za kijamii.
Tufuatilie kwenye mitandao yetu ya kijamii
INSTAGRAM - / elctned
FACEBOOK ACCOUNT North Eastern Diocese
FACEBOOK PAGE - ELCT-North Eastern Diocese
YOUTUBE - / KKKT DKMS Online TV
WEBSITE: www.elctned.org
KWA MAONI NA USHAURI:
Simu : +255 743 399 798
- Hits: 2086
Uongozi Bora: Askofu Dkt. Mbilu Aweka Mkazo kwenye Stahiki za Watumishi wa Dayosisi
- Details
![]()
Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania, Dayosisi ya Kaskazini Mashariki (KKKT-DKMs), Dkt. Msafiri Joseph Mbilu, ametoa pongezi za dhati kwa Wainjilisti Wanaume wa Dayosisi kwa huduma yao na uaminifu katika kuitenda kazi shambani mwa Bwana.
Akizungumza tarehe 28/11/2025 wakati akifungua semina maalum inayowakutanisha Wainjilisti wanaume wa KKKT-DKMs katika Usharika wa Korogwe, Askofu Dkt. Mbilu alisisitiza kuwa uongozi wa Dayosisi unatambua, kuthamini na kulinda mchango muhimu wa Wainjilisti katika kukuza na kuimarisha kundi la Mungu.
Aliongeza kuwa nguvu, hekima na kujitoa kwao kunaleta matokeo na ustawi si tu katika Kanisa bali hata katika jamii wanazozihudumia.
Kwa msisitizo wa kipekee Askofu Dkt. Mbilu ameonesha moyo wake wa kujali watumishi kwa kubainisha kuwa ataendelea kusimamia kwa karibu masuala yote yanayohusu ustawi na haki za watumishi wote katikadayosisi.
Ameahidi kuhakikisha stahiki mbalimbali zinaendelea kutolewa kwa wakati, ikiwemo michango ya NHIF na mifuko mingine ya kijamii, ili watumishi waendelee kufanya kazi kwa amani, uadilifu na matumaini huku akiitaka Ofisi ya Msaidizi wa Askofu kutoa mapema taarifa katika Ofisi ya Askofu punde Wainjilisti wanapokaribia kustaafu.
Askofu Dkt. Mbilu amesisitiza kuwa uongozi hauishii katika kuongoza tu, bali unajumuisha pia kuhakikisha kuwa wale wanaohudumu katika nafasi mbalimbali katika Dayosisi wanatunzwa, wanathaminiwa na kuwekewa mazingira bora ya kutekeleza huduma ikiwa hii ni sehemu ya wito wa Kristo wa kujenga, kuenzi na kutiana nguvu katika kuitenda kazi ya Bwana.
Tufuatilie kwenye mitandao yetu ya kijamii
INSTAGRAM - / elctned
FACEBOOK ACCOUNT North Eastern Diocese
FACEBOOK PAGE - ELCT-North Eastern Diocese
YOUTUBE - / KKKT DKMS Online TV
WEBSITE: www.elctned.org
KWA MAONI NA USHAURI:
Simu : +255 743 399 798
- Hits: 2292
Page 2 of 134

