ELCT North Eastern Diocese
MATUKIO KATIKA PICHA- Kutoka Usharika wa Źory nchini-Poland
- Details
Matukioa katika picha Ibada ya Jumapili ya tarehe 17/09/2023, katika Usharika wa Źory nchini Poland, ikiwa ni mwendelezo wa ziara ya Baba Askofu Dkt. Msafiri Joseph Mbilu, ambapo kutoka Bara la Afrika ni Mjumbe pekee kwenye Kamati ya Ibada na Muziki kwenye mkutano Mkuu wa Fungamano la Makanisa ya Kilutheri Duniani (LWF) unaoendelea nchini Poland .Wajumbe wa Mkutano huo wamepata nafasi ya kushiriki Ibada ya Jumapili kwenye sharika mbalimbali. Ujumbe mkuu wa Mkutano huu ni kutoka kitabu cha Waefeso 4:4-6 "MWILI MMOJA, ROHO MMOJA, TUMAINI MOJA".
- Hits: 507
Askofu Dkt. Mbilu kuongoza nyimbo za utamaduni wa Kiafrika Mkutano Mkuu wa LWF.
- Details


- Hits: 477
Askofu Dkt. Msafiri Mbilu, nyumbani kwa Dean Mstaafu Mzee Amasia Mweta.
- Details
Leo tarehe 02 Septemba,2023, Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, Mch Dkt. Msafiri Joseph Mbilu,amemtembelea Dean Mstaafu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki Mch. Amasia Mweta, nyumbani kwake Mpalalu-Bumbuli.
- Hits: 783
Ibada ya Kipaimara Jimbo la Kusini ,Usharika wa Irente.
- Details
Tarehe 27/08/2023 imekuwa siku ya baraka tele kwa washarika wa Jimbo la Kusini ,Usharika wa Irente kwani vijana wapatao 36 wamebarikiwa huku mmoja kati yao akibatizwa. Baba Askofu Dkt. Msafiri Joseph Mbilu ndiye aliyeongoza Ibada hiyo. Katika Risala ya vijana hao waliobarikiwa kwa Baba Askofu Dkt. Mbilu , wamekiri kufundishwa Biblia kwa ujumla wake , mtaala wa kitabu cha pokea chapa ya Kristo na vitabu vingine, katekisimo ndogo ya Martin Luther , nyimbo za Ibada na Liturgia katika kitabu cha Tumwabudu Mungu Wetu na kuahidi kuwa imani yao sasa ni thabiti na kamwe hawata tikiswa na ulimwengu na wataendelea kuwa wafuasi na wanafunzi chini ya mwalimu mkuu yaani Yesu Kristo hadi hapo atakaporudi kulichukuwa kanisa lake.
- Hits: 797
Page 2 of 91