ELCT North Eastern Diocese
Toggle Navigation
  • Home
  • Our Diocese
  • Wopa
  • Gallery
  • Institutions
    • Irente Children's Home
    • Irente School for the Blind
    • Rainbow School
    • Lwandai Secondary School
    • Lutindi Mental Hospital
    • Bangala Lutheran Junior Seminary
    • Bumbuli Hospital
    • SEKOMU university
    • Namna ya kuchangia kazi za maendeleo na Vituo vya kutoa huduma kwa watu wenye mahitaji maalumu (KKKT-DKMs)
  • Calendar
  • Projects
    • Irente Biodiversity Reserve
    • UTC - Usambara Technological Center
    • Restaurants and Hostels
      • Tumaini Mbuyukenda Hostel and Restaurant
      • Martin Luther Garden and Restaurant
      • Tumaini Songe Restaurant and Hostel
      • Hohen Restaurant and Hostel
      • Tumaini Lushoto Restaurant and Hostel
  • Superintendent
    • Coast Superintendent
    • Northern Superintendent
    • Southern Superintendent
    • Plains Superintendent
  • New-clips
  • Contact us
  • You are here:  
  • Home

Bishop Rev.Dr. Msafiri J. Mbilu

Change Language

English German Spanish Swahili Swedish

News & Updates

  • TANGAZO LA NAFASI MOJA YA KAZI MENEJA WA SHAMBA (FARM MANAGER) KITUO CHA IRENTE FARM

    TANGAZO LA NAFASI MOJA YA KAZI MENEJA WA SHAMBA (FARM MANAGER) KITUO CHA IRENTE FARM

    TANGAZO LA NAFASI YA KAZI Tarehe 19 Juni 1963, Kanisa la Usambara - Digo na makanisa mengine sita ya...
  • Askofu Dkt.Mbilu akutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi wa Uendeshaji  NSSF

    Askofu Dkt.Mbilu akutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi wa Uendeshaji NSSF

    Leo tarehe 01/04/2026, Askofu Dkt. Msafiri Joseph Mbilu amepokea ugeni kutoka Mfuko wa Taifa wa Hifa...
  • TAARIFA

    TAARIFA

    Uongozi wa KKKT – Dayosisi ya Kaskazini Mashariki ukiwakilishwa na Katibu Mkuu Mwl. Julius Madiga, u...
  • ASKOFU KKKT DAYOSISI YA KASKAZINI MASHARIKI AZINDUA BODI YA MFUKO WA PENSION

    ASKOFU KKKT DAYOSISI YA KASKAZINI MASHARIKI AZINDUA BODI YA MFUKO WA PENSION

    Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki. Dkt. Msafiri Jos...
  • Taarifa Ziara ya Botswana kwenye Mkutano wa UEM Kanda ya Afrika

    Taarifa Ziara ya Botswana kwenye Mkutano wa UEM Kanda ya Afrika

    Dayosisi yetu imepata heshima kubwa ya kushiriki katika Mkutano wa Kanda ya Afrika ulioandaliwa na U...

.



 

 

Staff Email

ELCT North Eastern Diocese

Wakurugenzi Wapya,Mkuu wa Jimbo KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki watambulishwa

  • Print
Details
Published: 13 May 2024

Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, Mch Dkt. Msafiri Joseph Mbilu amesema anaimani na wakurugenzi wapya waliochaguliwa hivi karibuni kusimamia Kurugenzi mbalimbali za Dayosisi huku akiwataka waumini pamoja na wakuu wa vituo vya Dayosisi kuwapa ushirikiano ili waweze kutimiza malengo yanayokusudiwa.



Askofu Dkt. Mbilu, ameyasema hayo katika Ibada ya Jumapili ya tarehe 12/05/2024 iliyofanyika katika Jimbo la Tambarare Usharika wa Korogwe na kuongeza kuwa sasa Kurugenzi zote za Dayosisi zimekamilika kwakuwa na Wakurugenzi wenye sifa baada ya nafasi hizo kukaimiwa kwa kipindi kirefu, hivyo anaamini Wakurugenzi hao utendaji wao wa kazi utaleta matokeo chanya na manufaa kwa Dayosisi.

Wakurugenzi hao wapya ni Mkurugenzi wa Uchumi, Mipango na Maendeleo Bibi, Pendo Wilfred Lauwo na Mkurugenzi wa huduma za jamii Bw. Afizai Vuliva. Aidha Baba Askofu amemtambulisha Rasmi Mkuu wa Jimbo Mteule wa Jimbo la Tambarare Mch. John Ndimbo na hivyo kumtakia baraka za Mungu katika utendaji wake wa kazi huku akimtaka kuendeleza mambo mazuri aliyoyafanya mtangulizi wake Mch. Frank Mtangi. Mch. John Ndimbo amechukuwa nafasi ya kuliongoza Jimbo la Tambarare baada ya Mtangulizi wake Mch. Frank Mtangi kuhamishiwa Jimbo la Pwani.

Ibada hii iliyoambatana na matendo mbalimbali pia Washarika wa Usharika wa Korogwe waliitumia Ibada hiyo kuungana na Wanadayosisi kwa ujumla kumuombea na kumtakia heri na baraka Baba Askofu Dkt. Mbilu, kufuatia kufikisha miaka Mitatu (3) toka kuingizwa kazini.

Ikumbukwe kuwa Baba Askofu Dkt. Msafiri Joseph Mbilu, aliingizwa kazini katika Ibada iliyofanyika Kanisa Kuu Lushoto tarehe 09/05/2021, na kisha yeye kumuingiza kazini msaidizi wake, Mch. Michael Mlondakweli Kanju hivyo 09/05/2024 alitimiza miaka hiyo mitatu ya kuiongoza KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki.

Hits: 10167

Miaka mitatu ya Uongozi wa Baba Askofu Dkt. Msafiri Joseph Mbilu

  • Print
Details
Published: 09 May 2024

Mei 9 mwaka 2021 ilikuwa ni siku iliyotawaliwa na nderemo, vifijo na shamrashamra katika viunga vya Lushoto, siri nyuma ya furaha hii si nyingine bali ni historia mpya kuandikwa, wakristo wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki walipata Askofu mpya, kiongozi ambae atayabeba maono na dira ya KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki huyu sio mwingine bali ni Askofu Dkt. Msafiri Joseph Mbilu.

Baba Askofu Dkt. Mbilu, aliingizwa kazini katika Ibada iliyofanyika Kanisa Kuu Lushoto tarehe 09/05/2021, na kisha yeye kumuingiza kazini msaidizi wake, Mch. Michael Mlondakweli Kanju. sasa leo tarehe 09/05/2024 ni miaka mitatu ya Uongozi wa Baba Askofu Dkt. Msafiri Joseph Mbilu tangu alipopewa kibali na Mungu cha kuiongoza KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki.
 
Leo tarehe 09/05/2024 zimetimia siku 1,096, yaani miaka mitatu tangu alipoingizwa kazini kushika wadhifa huo , bado tunaiona shauku ileile ndani yake kwani licha ya kusimamia mafundisho sahihi ya Neno la , Askofu Dkt. Mbilu amesimamia msingi wa Dayosisi katika kumhudumia mwanadamu kimwili, kiakili na kiroho.

Askofu Dkt. Mbilu licha ya kusimamia Dayosisi kupitia kauli mbiu yake ya kasi tofauti, ameendelea kuwa mnyenyekevu na msikivu kwa washarika wote  kwani anaamini ushirikiano mzuri wanaompa ndio msingi wa mafaniko ya Dayosisi.

 
Hits: 9474

Sinodi rafiki ya Southeastern Pennsylvania yapata Askofu mpya Congratulations Bishop-elect Penman!

  • Print
Details
Published: 05 May 2024
Askofu Dkt. Msafiri Joseph Mbilu, pamoja na msaidizi wake Mch. Michael Kanju, wameshiriki kwenye uchaguzi wa kumpata Askofu Mpya wa Sinodi rafiki ya Southeastern Pennsylvania, iliyoko Philadelphia nchini Marekani , ambapo uchaguzi huo uliofanyika leo tarehe 05/05/2024 umekamilika na Mch. Bryan Penman amechaguliwa kuwa Askofu Mteule akichukuwa nafasi ya mtangulizi wake
 Askofu Dkt. Patricia Davenport aliyemaliza muda wake.

Katika uchaguzi huo Askofu Mteule Mch. Penman amepata ushindi dhidi ya mshindani wake wa karibu Mch. Karl Richard.
Hits: 8599

Read more ...

Ziara ya kikazi ya Baba Askofu Dkt. Msafiri Joseph Mbilu nchini Marekani tarehe 26-04 hadi 08-05.2024

  • Print
Details
Published: 02 May 2024

Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, Mch Dkt. Msafiri Joseph Mbilu, anaendela na ziara yake ya kikazi iliyoanza tarehe 26/04/2024 nchini Marekani katika Mji wa Philadelphia, ambako ndiko Makao Makuu ya Synod rafiki ya Southeastern Pennsylvania yalipo. Hii ni mojawapo ya Synod za Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Marekani.

Hits: 8747

Read more ...

  1. Kutoka Usharika wa Mikanjuni Tanga
  2. Mwendelezo wa  ziara  ya Askofu Dkt. Mbilu  kutembelea Jimbo la Pwani na Sharika
  3. Tamati ziara ya Askofu Dkt. Mbilu Jimbo la Pwani
  4. Askofu Henrik Stubkjæ atoa wito kupima Afya mara kwa mara

Page 29 of 137

  • 24
  • ...
  • 26
  • 27
  • 28
  • 29
  • ...
  • 31
  • 32
  • 33

Back to Top

© 2026 ELCT North Eastern Diocese