ELCT North Eastern Diocese
Toggle Navigation
  • Home
  • Our Diocese
  • Wopa
  • Gallery
  • Institutions
    • Irente Children's Home
    • Irente School for the Blind
    • Rainbow School
    • Lwandai Secondary School
    • Lutindi Mental Hospital
    • Bangala Lutheran Junior Seminary
    • Bumbuli Hospital
    • SEKOMU university
    • Namna ya kuchangia kazi za maendeleo na Vituo vya kutoa huduma kwa watu wenye mahitaji maalumu (KKKT-DKMs)
  • Calendar
  • Projects
    • Irente Biodiversity Reserve
    • UTC - Usambara Technological Center
    • Restaurants and Hostels
      • Tumaini Mbuyukenda Hostel and Restaurant
      • Martin Luther Garden and Restaurant
      • Tumaini Songe Restaurant and Hostel
      • Hohen Restaurant and Hostel
      • Tumaini Lushoto Restaurant and Hostel
  • Superintendent
    • Coast Superintendent
    • Northern Superintendent
    • Southern Superintendent
    • Plains Superintendent
  • New-clips
  • Contact us
  • You are here:  
  • Home

Bishop Rev.Dr. Msafiri J. Mbilu

Change Language

English German Spanish Swahili Swedish

News & Updates

  • TANGAZO LA NAFASI MOJA YA KAZI MENEJA WA SHAMBA (FARM MANAGER) KITUO CHA IRENTE FARM

    TANGAZO LA NAFASI MOJA YA KAZI MENEJA WA SHAMBA (FARM MANAGER) KITUO CHA IRENTE FARM

    TANGAZO LA NAFASI YA KAZI Tarehe 19 Juni 1963, Kanisa la Usambara - Digo na makanisa mengine sita ya...
  • Askofu Dkt.Mbilu akutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi wa Uendeshaji  NSSF

    Askofu Dkt.Mbilu akutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi wa Uendeshaji NSSF

    Leo tarehe 01/04/2026, Askofu Dkt. Msafiri Joseph Mbilu amepokea ugeni kutoka Mfuko wa Taifa wa Hifa...
  • TAARIFA

    TAARIFA

    Uongozi wa KKKT – Dayosisi ya Kaskazini Mashariki ukiwakilishwa na Katibu Mkuu Mwl. Julius Madiga, u...
  • ASKOFU KKKT DAYOSISI YA KASKAZINI MASHARIKI AZINDUA BODI YA MFUKO WA PENSION

    ASKOFU KKKT DAYOSISI YA KASKAZINI MASHARIKI AZINDUA BODI YA MFUKO WA PENSION

    Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki. Dkt. Msafiri Jos...
  • Taarifa Ziara ya Botswana kwenye Mkutano wa UEM Kanda ya Afrika

    Taarifa Ziara ya Botswana kwenye Mkutano wa UEM Kanda ya Afrika

    Dayosisi yetu imepata heshima kubwa ya kushiriki katika Mkutano wa Kanda ya Afrika ulioandaliwa na U...

.



 

 

Staff Email

ELCT North Eastern Diocese

Tunzeni miundombinu ya Hospital hii

  • Print
Details
Published: 06 July 2024
HABARI KWA UFUPI.
Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, Mch Dkt. Msafiri Joseph Mbilu, amemshukuru na kumpongeza Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt.Samia Suluhu Hassan, kwa kuendelea kuwajali na kuwahudumia Wananchi katika sekta ya Afya kwa kujenga Hospital kubwa ya Wilaya ya Handeni iliyopo katika Kijiji cha Mkata, kwa kushirikiana na wadau wengine wa maendeleo kutoka ndani na nje ya Nchi.
Hits: 8629

Read more ...

Siku ya pili , Mkutano wa Wachungaji na Mashemasi KKKT- Dayosisi ya Kaskazini Mashariki

  • Print
Details
Published: 05 July 2024

KATIKA PICHA: Siku ya pili , Mkutano wa Wachungaji na Mashemasi KKKT- Dayosisi ya Kaskazini Mashariki Mkutano huu unafanyika katika Jimbo la Magharibi Usharika wa Mkata . Leo tarehe 05/07/2024 zimewasilishwa mada kutoka kwa wawezeshaji pamoja na taarifa mbalimbali kutoka kwenye Kurugenzi za Dayosisi.

 

 

Hits: 8616

Wachungaji pamoja na Mashemasi wakumbushwa juu ya utumishi wao.

  • Print
Details
Published: 04 July 2024

Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania Dayosisi ya Kaskazini Mashariki Mch Dkt. Msafiri Joseph Mbilu, amewakumbusha Wachungaji pamoja na Mashemasi juu ya wito walioitiwa katika kumtumikia Mungu kwa uaminifu wote.

Askofu Dkt. Mbilu ametoa wito huo tarehe 04/07/2024 akiwa anafungua mkutano wa Wachungaji na Mashemasi unaofanyika katika Jimbo la Magharibi Usharika wa Mkata ulioandaliwa na Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania Dayosisi ya Kaskazini Mashariki na kusema kua kila Mtumishi ano wajibu wa kutumika sawa sawa na wito ambo Mungu amemuitia.

Hits: 9099

Read more ...

Waziri Ofisi ya Rais Uwekezaji na Mipango awahimiza Wajumbe wa Mkutano wa Halmashauri Kuu ya CCT kujikita katika uwekezaji

  • Print
Details
Published: 03 July 2024

Waziri Ofisi ya Rais Uwekezaji na Mipango Mhe. Prof. Kitila Mkumbo,ameihamasisha Jumuiya ya Kikristo Tanzania ambayo inajulikana kwa kifupi (CCT) kujikita katika swala zima la Uwekezaji katika nyanja mbalimbali kama vile Kilimo Viwanda na Utalii kwani Serikali imefungua milango mingi ya Uwekezaji katika kipindi hiki.
Prof. Kitila Mkumbo ambaye ndiye aliyekuwa Mgeni Rasmi kwenye Mkutano huo wa 58 wa Halmashauri Kuu ya CCT uliofanyika tarehe 03/07/2024, katika Mkutano huo uliofanyika katika kituo kinachomilikiwa na CCT, cha Morogoro Women Training Center (MWTC).
Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, Mch Dkt. Msafiri Joseph Mbilu, ni mmoja wa wajumbe walioshiriki katika mkutano huu,mbali na Baba Askofu Mkutano huu pia ulihudhuriwa na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Morogoro mjini.

Jumuiya ya Kikristo Tanzania ambayo inajulikana kwa kifupi kama CCT (Christian Council of Tanzania), ni Taasisi ya Ki-ekumene inayowakilisha Umoja wa Madhehebu ya Kikristo ya Kiprotestanti. Kwa sasa CCT inaundwa na Makanisa mbalimbali Wanachama na Vyama vya Kikristo au vyenye mwelekeo wa kikanisa kutoka Tanzania Bara na Visiwani. Taasisi hii ilianzishwa rasmi tarehe 23 Januari, 1934 kutokana na maono ya Wamisionari kutoka Kanisa Anglikana, Kanisa la Moravian na Kanisa la Kiinjili la Kilutheri. Wamisionari hawa walipata maono ya kujenga umoja kati ya makanisa wanachama ambao utajihusisha na masuala mbalimbali ya ki-imani, kimaendeleo na kijamii. Muungano huu ulijulikana kwa jina la Kiingereza, Tanganyika Missionary Council (TMC).


Mnamo mwaka 1964 Mungu aliwapa maono watumishi wake Baba Askofu Stephano Reuben Moshi (Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania), Baba Askofu Theofilo Kisanji (Kanisa la Moravian Tanzania) na Baba Askofu Mkuu John Sepeku (Kanisa Anglikana Tanzania) kubadilisha usajili wa TMC kuwa Christian Council of Tanzania (CCT), jina linalotumika hadi sasa. Idadi ya Makanisa yaliyopo chini ya CCT imekuwa ikiongezeka kutoka Makanisa matatu (3) ya mwanzo mwaka 1934 hadi kufikia makanisa ya Kiprotestanti kumi na mbili (12) yaliyopo mwaka 2021.


Kwa sehemu kubwa Makanisa Wanachama wa CCT yanafuata mapokeo ya Makanisa ya Kiinjili. Aidha, ili kuwezesha kukua na kuimarika kwa umoja wa kweli, Makanisa Wanachama yanatumia utaratibu unaofanana katika mambo muhimu. Mambo hayo ni pamoja na Ukiri wa Imani ya Mitume (Apostles Creed), Ukiri wa Imani ya Nikea (Nicene Creed) katika kuendeleza ufalme wa Mungu kwa njia ya mahubiri na kuunganishwa kuwa mwili mmoja katika Yesu Kristo.

Hits: 8437
  1. Askofu Dkt. Mbilu aongoza Ibada ya Kustaafu kwa Heshima kwa Mchungaji Shemkala
  2. Ibada ya Kipaimara Usharika wa Mlalo , Youths Confirmation at Mlalo Lutheran Parish.23/06/2024
  3. Ziara ya Baba Askofu Dkt. Mbilu katika Taasisi ya Elimu ya Kolowa Technical Training Institute (KOTETI)
  4. Askofu Dkt. Mbilu azindua Usharika wa Bethania uliopo katika Jimbo la Pwani.

Page 25 of 137

  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
  • 26
  • 27
  • 28
  • 29

Back to Top

© 2026 ELCT North Eastern Diocese